ZINAZOVUMA:

TOGO: Upinzani wagomea mabadiliko ya katiba

Upinzani nchini Togo umekataa mabadiliko ya katiba nchini humo na...

Share na:

Wanaharakati na viongozi wa upinzani nchini Togo walitoa tamko siku ya Jumatano (Machi 27) katika maandamano ya kumtaka rais Faure Gnassingbé kutia saini katiba mpya. Mabadiliko hayo ya katiba yangefutalia mbali uchaguzi ujao wa urais na kurefusha utawala wa rais wa sasa.

Katiba hiyo inayosubiri kutiwa saini na Rais Gnassingbé wa Togo, ilipitishwa na wabunge wa nchi hiyo mapema wiki hii, imelipa bunge mamlaka ya kuchagua rais, na kuondoa uchaguzi wa moja kwa moja.

Hii inaongeza uwezekano wa Gnassingbé kuchaguliwa tena mamlaka yake yatakapokoma mwaka 2025.

Baadhi ya wataalamu wa masuala ya sheria wanasema kuwa katiba kwa hakika inaweka vikwazo kwa mamlaka ya marais wajao, kwani inaleta ukomo wa muhula mmoja na kukabidhi madaraka makubwa kwa mtu anayefanana na waziri mkuu anayeitwa rasmi rais wa baraza la mawaziri.

Lakini upinzani unahofia kuwa jukumu hilo linaweza kuwa njia nyingine kwa Gnassingbé kuongeza nguvu zake kwenye mamlaka.

Hakika, rais wa baraza la mawaziri aidha atakuwa “kiongozi wa chama kinachopata wabunge wengi wakati wa uchaguzi.” Au kiongozi wa muungano wa vyama unaoshinda.

Rais wa baraza la mawaziri atatawala kwa muhula wa miaka sita bila kikomo cha muhula.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya