ZINAZOVUMA:

Sonko kugombea Urais wa Senegal 2024

Ousmane Sonko arudishwa katika orodha ya wagombea Urais kwa amri...

Share na:

Ousmane Sonko, kiongozi wa upinzani nchini Senegal, atangaza kugombea Urais mwezi Februari 2024.

Hata hivyo Sonko hakupatiwa nyaraka muhimu za kujaza kwa ajili ya kugomea Urais.

Sonko alitakiwa kuwsilisha uthibitisho wa kukusanya sahihi zakutosha ili aweze kugombea nafasi hiyo.

Mbali na kuwa taarifa hizo alitakiwa kukabidhi tarehe 26, hadi wiki iliyopita hakuwa amepata fomu hizo.

Pia Sonko alihukumiwa bila kuwepo mahakamani kufungwa miaka miwili kutokana na makosa ya unyanyasaji kwa vijana.

Baadhi ya wagombea wanaotarajia kupokea kijiti cha Urais wa Senegal kutoka kwa Macky Sall (Chini Kushoto), Aminata Toure (Juu Kushoto), Ousmane Sonko (juu Kulia) na Bassirou Faye (chini Kulia).

Hata hivyo mgombea huyo mtarajiwa amekaa jela kwa miezi kadhaa kwa makosa mbalimbali yakiwemo kujihusisha na vikundi vya kigaidi, Uasi na hata kuhatarisha usalama wa taifa hilo.

Mwanasiasa huyo alirudishwa katika orodha ya wagombea wa Urais, baada ya amri kutoka kwa mahakamani mwezi Disemba. Pia mfuasi wake wake Bassirou Doimaye Faye kutokea gerezani amewasilisha ombi la kugombea uchaguzi huo.

Mgombea mwingine wa Urais ni Aminata Toure ambaye alikuwa waziri Mkuu na mshirika wa Mack Sally, anayegombea tena Urais.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya