ZINAZOVUMA:

Sonko kuharibu uchaguzi Senegal

Kiongozi wa upinzani nchini Senegal amesema atavuruga uchaguzi wa mwakani...
Senegalese's opposition leader Ousmane Sonko, charged with rape, talks to media at his party's headquarters in Dakar on March 8, 2021 after being freed from detention. - Senegal's main opposition leader called for "much larger" protests, but urged non-violence after days of deadly clashes in the West African state sparked by his recent arrest. (Photo by Seyllou / AFP)

Share na:

Kiongozi wa upinzani wa Senegal, Ousmane Sonko, hana mpango wa kutafuta maridhiano na Rais Macky Sall, na ameshiria kuwa anaweza kuvuruga uchaguzi wa mwaka ujao, ikiwa hataruhusiwa kugombea.

“Hakutakuwa na uchaguzi katika nchi hii, iwapo Rais Macky Sall atapinga kugombea kwangu,” Sonko alisema hayo akiwa nyumbani kwake katika mji mkuu wa Dakar ambako amekuwa chini ya kizuizi cha nyumbani tangu alipohukumiwa kifungo cha miaka miwili mwezi Juni, kwa mashtaka yaliyotokana na madai ya ubakaji.

Sonko alikanusha mashtaka hayo na kusema kuwa yanalenga kumzuia kushiriki katika uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika mwezi Februari mwakani.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya