ZINAZOVUMA:

Matokeo ya Awali – Uchaguzi Mkuu wa Senegal

Bassirou Diomaye Faye anaongoza mbio za urais Senegal kama ilivyotangazwa...
FILE PHOTO: A supporter of jailed Senegalese opposition leader Ousmane Sonko reacts during an electoral campaign caravan to support the detained presidential election candidate Bassirou Diomaye Faye, who Sonko picked to replace him in the race, in the outskirts of Dakar, Senegal March 12, 2024. REUTERS/Zohra Bensemra/File Photo

Share na:

Nchi nzima ya Senegal iko roho juu wakingoja matokeo ya uchaguzi wa rais wa 2024. Wakati yakingojwa matokeo ya jumla tayari yameanza kutoka matekoe ya awali yanayoonyesha Diomaye akiongoza kwa asilimia zaidi ya 50.

Hii inaonyesha nchi imewaamini Diomaye na Sonko hadi wanapindua meza mbele ya chama tawala nchini humo.

Takwimu zilizokusanywa uwanjani na Alphonse Diombo Thiakane, mtaalamu wa takwimu wa Radio Futurs Médias (RFM), zimefunua mielekeo ya kwanza katika matokeo haya:
Bassirou Diomaye Faye: 56.13%
Amadou Ba: 31.4%
Khalifa Ababacar Sall: 4.0%
Aliou Mamadou Dia: 3.13%
Idrissa Seck: 1.6%

Kiongozi wa Upinzani Ousmane Sonko nyuma ya Mgombea Urais Bassirou Diomaye Faye mwenye nguo nyeupeMachi 16 2024 katika kampeni nchini Senegal. (MUHAMADOU BITTAYE / AFP)

Inapaswa kuzingatiwa kwamba takwimu hizi zinawakilisha mielekeo ya awali na matokeo rasmi yatathibitishwa baadaye na mamlaka husika za uchaguzi.

Hata hivyo, ishara hizi za mapema zinaonyesha mandhari ya kisiasa inayobadilika na ushiriki mkubwa wa wapiga kura.

Mbali na mahakama mwezi Disemba kutoa amri ya Sonko kuwepo katika wagombea wa uchaguzi mwaka huu, hajaonekana katika wagombea na badala yake mwenzake amevuruga safu ya ulinzi ya chama tawala nchini Senegal.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya