ZINAZOVUMA:

Bashungwa awataka wamiliki wa shule kutoa elimu ya kujiokoa

Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa atoa wito kwa wamiliki wa...

Share na:

Waziri Innocent Bashungwa wa Ujenzi nchini, ametoa wito kwa viongozi na wasimamizi wa shule za serikali na binafsi kutoa elimu kuhusu matukio ya dharura yanayoweza kutokea katika mazingira ya shule.

Bashungwa ameyasema hayo wakati alipozindua Bweni la wavulana katika shule ya msingi ya kiingereza KARADEA, katika kata ya Bugene wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.

Aidha Waziri Bashungwa amelipongeza shirika la KARADEA, kwa kuendelea kufanya uwekezaji katika shule hiyo na ameahidi kuwa serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi ambazo zimeendelea kuwa na mchango mkubwa kwa jamii ya watanzania.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya