ZINAZOVUMA:

TETEMEKO LAPITA MEXICO, MAREKANI IMESALIMIKA

Tetemeko latokea Mexico katika Ghuba ya California, inayopakana na fukwe...

Share na:

Katika ghuba ya California nchini Mexico imepigwa na tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 6.4 siku ya Jumapili, kwa mujibu wa Kituo cha Seismolojia cha Ulaya na Bahari ya Mediterranean (EMSC). Inasemekana kuwa tetemeko hilo limetokea katika kina cha kilomita 10 (maili 6.21) kutoka katika mgongo wa ardh, kutokana na vipimo vya EMSC.

Ofisi ya ulinzi wa raia ya Mexico imethibitisha kwamba hakuna ripoti za haraka za uharibifu katika maeneo ambapo tetemeko hilo lilisikika, lakini imependekeza mashua na idadi ya watu wanaoishi katika maeneo ya pwani kuchukua tahadhari kutokana na mawimbi yanayotarajiwa katika bandari.

Onyo hili kwa wakazi wa pwani za ghuba hiyo na maeneo mengine ya pwani iliyofikiwa na tetemeko hilo ni kutokana na kutegemewa kuwa na mabadiliko ya kina cha maji ya bahari katika maeneo hayo.

Muda mfupi baada ya tetemeko kutokea, mfumo wa Tsunami wa Marekani ulisema kwamba hakuna hatari ya Tsunami katika Pwani ya Magharibi ya Marekani, Columbia ya Uingereza, au Alaska. Maeneo haya yote yanapatikana kaskazini mwa Ghuba hiyo iliyokumbwa na tetemeko.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya