ZINAZOVUMA:

Raisi wa FIFA aipongeza Yanga

Raisi wa shirikisho la mpira duniani FIFA aipongeza klabu ya...
FIFA President Gianni Infantino arrives on the pitch at the end of during the FIFA Club World Cup final football match between Spain's Real Madrid and Saudi Arabia's Al-Hilal at the Prince Moulay Abdellah Stadium in Rabat on February 11, 2023. (Photo by Fadel Senna / AFP)

Share na:

Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Gianni Infantino ameipongeza klabu ya Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2022/23.

Katika salamu zake za pongezi alizoandika kupitia kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Wallace Karia amesema siyo rahisi kutwaa ubingwa huo pasipo bidii ya timu nzima, ari na kujitolea.

Infantino ametoa pongezi kwa wote waliohusika katika kufanikisha klabu hiyo kufikia mafanikio hayo akiongeza kuwa kila mmoja anaweza kujivunia kwa hilo.

Aidha, ameipongeza TFF kwa mchango wake katika maendeleo na ustawi wa soka la Tanzania na Afrika kwa ujumla.

(Photo by Fadel Senna / AFP)

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya