ZINAZOVUMA:

Rais wa Cameroon afanya mabadiliko ya jeshi akihofia kupinduliwa

Raisi wa Cameroon Paul Biya amefanya mabadiliko katika Wizara ya...

Share na:

Raisi wa Cameroom Paul Biya amefanya mabadiliko katika Wizara ya Ulinzi na kuwateua viongozi wapya wa kijeshi mara baada tu ya mapinduzi yaliyofanyika nchini Gabon.

Biya ni mmoja wa marais waliokaa madarakani kwa muda mrefu zaidi barani Afrika. Hakuna sababu iliyotolewa kuhusu hatua hiyo ya mabadiliko hayo makubwa ya ghafla yaliyofanyika

Hata hivyo Kanali Cyrille Guemo, Mkurugenzi wa mawasiliano katika Wizara ya Ulinzi ya Cameroon, amesema kwamba uteuzi huo mpya ulikua kwenye mipango ya Rais kwa siku nyingi.

Lakini kutokana na hali ya mapinduzi ya kijeshi ambayo yanaenea katika mataifa ya Afrika Magharibi, viongozi ambao wamekuwa madarakani kwa muda mrefu sana wameingiwa na wasiwasi.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wamesema kizazi cha vijana ambacho kinaundwa na viongozi wa kijeshi hakivumilii tawala zinazofanya kazi kutakana na nasaba zao.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya