ZINAZOVUMA:

Raia wa Poland akamatwa katika njama ya kumuua Zelensky

Raia wa Poland akamatwa akihusishwa na njama za Urusi kutaka...

Share na:

Mwanaume mmoja raia wa Poland ameshtakiwa kwa madai ya kushirikiana na Urusi katika mipango ya kumuua Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky. kulingana na mamlaka nchini Ukraine na Poland.

Tuhuma hizo amepewa na mamlaka za Ukraine na Poland.

Taarifa kutoka Poland zinasema mwanamume anayeitwa Paweł K alipewa jukumu la “kusaidia, kati ya mambo mengine, katika kupanga na huduma maalum za Urusi kwa shambulio linalowezekana dhidi ya maisha ya mkuu wa nchi ya kigeni – Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky,” kama kwa taarifa ya Alhamisi (Aprili 18).

Kulingana na waendesha mashtaka, mwanamume huyo alipanga kutoa taarifa za usalama wa Uwanja wa Ndege wa Rzeszow-Jasionka uliopo Kusini Mashariki mwa Poland kwa majasusi wa Kirusi.

Pia uwanja huo upo takriban kilomita 100 kutoka katika mpaka wa Poland na Ukraine, na kufahamika kuwa ni moja ya viwanja vya ndege anavyotumia Zelensky kwa safari za nje.

Mwendesha mashtaka mkuu wa Ukraine Andriy Kostin alisema kuwa mshukiwa huyo anadaiwa “alianzisha mawasiliano” na wawakilishi wa jeshi la Urusi na “kuwajulisha utayari wake wa kushirikiana” na shirika la kijasusi la kijeshi la kigeni la Shirikisho la Urusi.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya