ZINAZOVUMA:

Marekani yawawekea vikwazo vipya Urusi

Marekani yaiwekea vikwazo vipya Urusi ambavyo vitawasilishwa katika mkutano wa...
U.S. President Joe Biden, Germany's Chancellor Olaf Scholz, Britain's Prime Minister Rishi Sunak, European Commission President Ursula von der Leyen, President of the European Council Charles Michel, Italy's Prime Minister Giorgia Meloni, Canada's Prime Minister Justin Trudeau, France's President Emmanuel Macron and Japan's Prime Minister Fumio Kishida attend a working lunch meeting at G7 leaders' summit in Hiroshima, western Japan May 19, 2023, in this handout photo released by Ministry of Foreign Affairs of Japan. Ministry of Foreign Affairs of Japan/HANDOUT via REUTERS

Share na:

Nchi ya Japan ndio mwenyeji wa mkutano wa mataifa ya G7 ambao unafanyika kuanzia leo tarehe 19 mpaka tarehe 21, ambao unahudhuriwa na viongozi wa nchi za Canada, Italy, France, Germany, Uingereza pamoja na marekani.

Huu ni mkutano wa pili wa G7 kutawaliwa na uvamizi wa Ukraine, na huku usiku kucha wa kuamkia leo kampeni za uvamizi wa anga ya Urusi ziliendelea.

Hata hivyo mkutano huo wa G7 umezindua vikwazo vipya dhidi ya nchi ya Urusi ambavyo vimewasilishwa na Taifa la Marekani.

Aidha taarifa zinasema kuwa Raisi wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy anatarajia kuhudhuria mkutano huo wa G7 ili kujadili uvamizi uliofanywa na Urusi nchini kwake.

Awali ilisemekana kuwa angejumuika nao kwa njia ya mtandao lakini taarifa mpya zinaeleza kuwa Raisi huyo atajumuika katika mkutano huo yeye mwenyewe na kuonana na viongozi wa G7 ana kwa ana.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya