ZINAZOVUMA:

Kesi ya Makonda na Lemutuz yafutwa

Kesi ya Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es...

Share na:

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imefuta shauri la madai lililofunguliwa na mfanyabiashara Patrick Kamwelwe dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mwenzake William Malecela ‘Lemutuz’.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Richard Kabate baada ya kukubali ombi la mawakili wa Makonda la kufutwa kwa shauri hilo kutokana na mdai kutoonekana mahakamani.

Akiwasilisha ombi hilo, Wakili wa Makonda, Gift Joshua amesema mdai hajaonekana mahakamani kwa mara ya nne mfululizo pamoja na wakili wake, hivyo kuiomba mahakama kuondoa shauri hilo.

Kamwelwe alifungua kesi dhidi ya Makonda akidai kuporwa gari aina ya Range Rover ambalo alimkabidhi Lemutuz ampatie Makonda ili alitumie wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa wiki mbili kisha amrudishie.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya