ZINAZOVUMA:

Kanisa Katoliki: Watanzania wawasaidie wahitaji

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam wawaasa watanzania...

Share na:

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es salaam limewataka Watanzania kujitolea katika kuwasaidia makundi mbalimbali ya kijamii hasa yenye uhitaji zaidi sambamba na kuzingatia ushauri wa kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuimarisha Afya kukabiliana na Magonjwa mbalimbali.

Hayo yamesemwa na Askofu Mkuu Jimbo la DSM, Juda Thadeues Ruwai’chi mbele ya Waandishi wa Habari wakati wa ufunguzi wa mbio za PUGU MARATHON 2024 mbio ambazo zenye kuwakutanisha Watu mbalimbali.

“Lengo kuu ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kukarabati Kituo cha Hija Pugu, Nyumba ya Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere aliyoishi wakati akifundisha Pugu Sekondari na kuboresha Maktaba ya Shule hiyo ya Pugu,” amesema Askofu Ruwaichi.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya