ZINAZOVUMA:

India na UAE zakubaliana kutumia sarafu moja

India na Umoja wa Falme za Kiarabu zimekubaliana kufanya biashara...

Share na:

India na Umoja wa Falme za Kiarabu wameingia makubaliano ambayo yanaruhusu biashara kati ya nchi hizo mbili kufanyika kwa kutumia sarafu ya India badala ya dola za Marekani.

Mataifa hayo mawili yamekubaliana kuanzisha mfumo wa malipo halisi unaowezesha uhamisho wa fedha za kimataifa kwa urahisi, hivyo kukuza biashara isiyo na vikwazo na ushirikiano wa kiuchumi zaidi.

Biashara ya pande mbili kati ya India na Umoja wa Falme za Kiarabu ilifikia dola bilioni 84.5 sawa na trilioni 205.69 kuanzia Aprili 2022 hadi Machi 2023, hivyo kufanya makubaliano haya kuwa muhimu kwa uchumi wa nchi zote mbili.

Kwa kuruhusu biashara kufanyika kwa kutumia sarafu ya India, makubaliano hayo yanapunguza gharama za uendeshaji biashara na ubadilishaji wa fedha ambazo zinaweza kuwa kubwa na kuchelewesha shughuli za biashara.

Hii inawapa wafanyabiashara na wawekezaji fursa ya kufanya malipo moja kwa moja kwa kutumia sarafu ya ndani, ambayo ni rahisi na yenye ufanisi zaidi.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya