ZINAZOVUMA:

Falme za Kiarabu kuisaidia Afrika mabadiliko tabia ya nchi

Nchi mbalimbali zimetoa ahadi ya kutoa pesa kuisaidia Bara la...

Share na:

Nchi kadhaa zimeahidi kutoa mamilioni ya dola kwa ajili ya juhudi za kuimarisha mfuko wa kusimamia shughuli za kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kufikia mwaka 2030.

Ahadi hizo zimetolewa katika mkutano wa kihistoria wa kilele kuhusu mazingira wa viongozi wa Kiafrika uliofunguliwa siku ya Jana na rais wa Kenya William Ruto.

Umoja wa Falme za Kiarabu umeahidi kutoa dola milioni 450 kwa ajili ya kusaidia miradi ya masoko ya Kiafrika ya upunguzaji viwango vya uzalishaji hewa ukaa.

Mradi wa masoko hayo ulianzishwa nchini Misri kufuatia mkutano wa kilele wa COP 27 mwaka jana.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya