ZINAZOVUMA:

Basi la Al-Saedy lapata ajari Tabora

Basi la Al-Saedy linalofanya safari zake kutoka Tabora kwenda Dar...

Share na:

Basi la Al-Saedy limepinduka alfajiri ya leo Jumatatu Agosti 7, 2023 katika Wilaya ya Uyui mkoani Tabora huku abiria wakipata majeraha akiwemo mmoja aliyevunjika mkono.

Basi hilo lilikuwa likielekea Dar es salaam kutoka Tabora ambalo liliondoka saa kumi na mbili asubuhi.

Diwani wa Kata ya Kigwa, Wilayani Uyui Bakari Kabata amesema ajali hiyo imetokea saa kumi na mbili na nusu kuelekea saa moja katika Kijiji cha Nzigala moja ya vijiji vilivyopo kwenye kata hiyo.

“Ajali imetokea na kujeruhi abiria akiwemo mmoja aliyevunjika mkono na hakuna aliyepoteza maisha,” amesema.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya