ZINAZOVUMA:

Utata wa wahusika shambulizi la ukumbi Moscow

Urusi inapeperusha bendera nusu mlingoti, huku ikizozana na Media za...

Share na:

Shambulizi lililotokea mjini Moscow limesababisha vifo 133 mpaka muda huu na wengi wakijeruhiwa. Shambulio hilo limetokea ikiwa ni siku chache baada ya Putin kushinda tena uchaguzi na kuendelea kuwa Rais wa nchi hio. Tukio hilo la aina yake linatajwa kuwa limeleta fedheha kwa jeshi la ulinzi wa Russia na pia kuleta majonzi na hasira kwa watu wa Russia. Rais wa taifa hilo kubwa duniani, Vladimir Putin ameapa atabainisha ni nani haswa wamehusika na atawahadhibu.

KWA AJILI GANI ANATAKA KUWABAINISHA NA ISIS WAMESEMA WAMEHUSIKA ?

Baada ya shambulizi watu waliofanya mauaji hayo kwa raia wa Urusi walionekana kutorokea Ukraine ila kabla hawajafanikisha walikamatwa. Rais Putin amedai kuwa haya mauaji yanahusishwa na Ukraine pamoja na mataifa ya magharibi. Rais wa Ukraine nae akaibuka akisema kuwa hashangazwi Putin kusema hivyo, baada ya kuangalia matatizo kwenye usalama wa nchi yake na alipofeli ila yeye anatafuta mahali pakupasemea

Media za magharibi zinashadadia kuwa ISIS ndio wamehusika na huku media za Urusi zikisema kuwa wanafanya hivyo makusudi ili wajifiche kwenye mwavuli wa ISIS ili wasigundulike.Media za magharibi zimeenda mbali zaidi zikionesha video ambazo ISIS wamezitoa kuwa wamehusika na hilo shambulio. Marekani ilisema kuwa ilimuonya Putin juu ya kuweza kutokea shambulio hilo ila Putin hakuchukulia maanani na kupuuzia.

Media za Mashariki ya kati wao wamedai template ya Telegram waliyotumia kama kielelezo cha kuwa ni ya ISIS ni ya muda sana na kwamba waliacha kuitumia muda sana.

Washutumia wamefikishwa mahakamani na kilichobakia ni kauli ya Putin ila kwa sasa nchi nzima ipo kwenye maombolezi na bendera zikiwa nusu mlingoti

UTATA WA UHUSIKAJI KUHUSU SHAMBULIZI WA UKUMBI WA MOSCOW

Shambulizi lililotokea mjini Moscow limesababisha vifo 133 mpaka muda huu na wengi wakijeruhiwa. Shambulio hilo limetokea ikiwa ni siku chache baada ya Putin kushinda tena uchaguzi na kuendelea kuwa Rais wa nchi hio. Tukio hilo la aina yake linatajwa kuwa limeleta fedheha kwa jeshi la ulinzi wa Russia na pia kuleta majonzi na hasira kwa watu wa Russia. Rais wa taifa hilo kubwa duniani, Vladimir Putin ameapa atabainisha ni nani haswa wamehusika na atawahadhibu.

KWA AJILI GANI ANATAKA KUWABAINISHA NA ISIS WAMESEMA WAMEHUSIKA ?

Baada ya shambulizi watu waliofanya mauaji hayo kwa raia wa Urusi walionekana kutorokea Ukraine ila kabla hawajafanikisha walikamatwa. Rais Putin amedai kuwa haya mauaji yanahusishwa na Ukraine pamoja na mataifa ya magharibi. Rais wa Ukraine nae akaibuka akisema kuwa hashangazwi Putin kusema hivyo, baada ya kuangalia matatizo kwenye usalama wa nchi yake na alipofeli ila yeye anatafuta mahali pakupasemea

Media za magharibi zinashadadia kuwa ISIS ndio wamehusika na huku media za Urusi zikisema kuwa wanafanya hivyo makusudi ili wajifiche kwenye mwavuli wa ISIS ili wasigundulike.Media za magharibi zimeenda mbali zaidi zikionesha video ambazo ISIS wamezitoa kuwa wamehusika na hilo shambulio. Marekani ilisema kuwa ilimuonya Putin juu ya kuweza kutokea shambulio hilo ila Putin hakuchukulia maanani na kupuuzia.

Media za Mashariki ya kati wao wamedai template ya Telegram waliyotumia kama kielelezo cha kuwa ni ya ISIS ni ya muda sana na kwamba waliacha kuitumia muda sana.

Washutumia wamefikishwa mahakamani na kilichobakia ni kauli ya Putin ila kwa sasa nchi nzima ipo kwenye maombolezi na bendera zikiwa nusu mlingoti

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya