ZINAZOVUMA:

Marumo Gallants wataka hamasa kama ya Raisi Samia

Mashabiki wa klabu ya Marumo Gallants wamtaka Raisi wa Afrika...

Share na:

Mashabiki wa timu ya Marumo Gallants ya nchini Afrika Kusini inayotarajiwa kucheza hatua ya nusu fainali dhidi ya Yanga ya nchini Tanzania imemuomba Raisi wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa kutoa hamasa kama anavyofanya Raisi wa Tanzania Samia Suluhu Hassani kwa timu zinazoshiriki michuano ya kimataifa.

Mtanzania anaeishi Afrika kusini amebainisha hilo wakati akifanya mahojiano na kituo cha “Azam TV” kuelekea katika mchezo wa nusu fainali ya shirikisho siku ya jumatano.

Ikumbukwe kuwa Raisi wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani alikua akitoa hamasa ya shilingi milioni 5 kwa kila goli katika hatua zilizopita na hivi karibuni alipandisha na kuahidi milioni 10 kuanzia hatua ya nusu fainali.

Yanga atakutana na Marumo Gallants tarehe 10 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam na baada ya wiki moja timu hizo zitarudiana katika ardhi ya Afrika Kusini.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya