ZINAZOVUMA:

Kenya: Lori laacha barabara na kuua watu 10.

Watu kumi wamepoteza maisha baada ya Lori kuacha njia na...

Share na:

Watu 10 wamepoteza maisha leo Jumamosi Aprili 8, 2023 katika Kaunti ya Migori nchini Kenya kutokana na ajali ya lori ambalo inaelezwa lilifeli breki na kuparamia kijiwe cha bodaboda.

Watu hao waliopoteza maisha inaelezwa ni vijana wa bodaboda waliokuwa wakisubiria wateja kwenye kijiwe chao.

Taarifa ya awali kupitia mtandao wa Tuko nchini Kenya imeeleza kuwa lori hilo la kubeba mchanga, lilipoteza mwelekeo na kugonga kundi la bodaboda ambao walikuwa pembezoni mwa barabara wakisubiri abiria.

Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema muda mfupi eneo hilo lilitapakaa damu na miili ya watu ambapo juhudi za kuwaokoa waliopata majeraja zilikuwa zinaendelea.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya