ZINAZOVUMA:

Eng. Hersi Mwenyekiti wa kwanza ACA

Eng. Hersi Said ateuliwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa chama...
Rais wa CAF Patrice Motsepe na Mwenyekiti wa ACA Hersi Said katika Mkutano mkuu wa Chama cha vilabu vya soka Afrika uliofanyika Marriott Mena House jijini Cairo, Egypt siku ya 30 November 2023 ©Weam Mostafa/BackpagePix

Share na:

Raisi wa klabu ya Yanga Eng. Hersi Said ateuliwa kushika nafasi ya mwenyekiti wa chama kipya cha Muungano wa klabu za Afrika (ACA).

Eng. Hersi ameteuliwa kushika nafasi hiyo kupitia mkutano ulofanyika, jijini Cairo nchini Misri siku ya Alhamisi.

Mkutano huo uliojumuisha viongozi wa vilabu vya soka takriban 60 kutoka afrika, huku Dr. Patrice Motsepe akiwa mwenyeji wa mkutano huo.

Huku Tanzania ikiwakilishwa na Eng. Hersi Said Aliyepata uenyekiti, pamoja na Salim Abdallah ‘Try Again’ mwenyekiti wa bodi ya Simba.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya