ZINAZOVUMA:

Zaidi ya watu 800 wanalala bila kula

Zaidi ya watu 800 wanalala bila kula kila siku kwa...

Share na:

Jana tarehe 28 Mei, 2023 ilikua ni siku ya njaa duniani ambapo takwimu zinaonesha kuna ongezeko la watu kutokupata mlo hata mmoja kwa siku.

Watu milioni 828 Duniani ambao ni takribani Asilimia 10 ya watu wote wanalala bila kula kila siku, ikiwa ni ongezeko la watu milioni 46 zaidi ya ilivyokuwa mwaka mmoja uliopita.

Takwimu hizo zimetolewa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mbili ya tatu ya watu hao ni Wanawake na 80% wanaishi katika maeneo yanayokabiliwa na mabadiliko ya hali ya hewa.

Ukiacha mbali na mabadiliko ya hali ya hewa sababu nyingne kubwa knayotajwa ni kuongezeka au kupanda kwa gharama za maisha hali inayopelekea watu kushindwa kumudu.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya