ZINAZOVUMA:

Uamuzi wa kuivamia Niger kujadiliwa leo

Viongozi wa kijeshi wa Jumuiya ya ECOWAS wanakutana leo nchini...
Members of the Armed Forces of Senegal discuss on the sidelines of the Economic Community of West African States (ECOWAS) Head of States and Government extraordinary session in Abuja, on August 10, 2023. West African leaders came together Thursday for an emergency summit on the coup in Niger, whose new military rulers have defied an ultimatum -- backed by the threat of force -- to restore the elected president and pressed ahead with appointing a new government. (Photo by KOLA SULAIMON / AFP)

Share na:

Wakuu wa Ulinzi wa Jumuiya ya ECOWAS wanakutana nchini Ghana leo Alhamisi na Ijumaa kukamilisha maandalizi ya kutumwa kwa Kikosi cha Kudumu cha kurejesha demokrasia nchini Niger.

Haya yanajiri kufuatia uamuzi wa wakuu wa nchi wa ECOWAS kukituma kikosi hicho baada ya juhudi za kidiplomasia kushindwa kuleta matokeo chanya ya kumrejesha madarakani Rais aliyeondolewa Mohamed Bazoum.

Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS inazidisha maradufu tishio lake la kuingilia kijeshi kurejesha utawala wa kikatiba nchini Niger baada ya serikali ya kijeshi kuchukua mamlaka mwezi uliopita.

Wakuu hao wa ulinzi wanakutana katika makao makuu ya jeshi la Ghana nchini Burma ili kupanga mkakati madhubuti wa hatua ya kijeshi nchini Niger.

Majadiliano hauo yatazingatia, rasilimali, idadi ya wanajeshi wanaohitajika, na utaratibu wa kawaida wa kufanya kazi kwa wanajeshi wa kivita.

Endelea Kusoma

Mwanzilishi wa Telegram mwenye asili ya kirusi amekamatwa nchini Ufaransa siku ya

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya