ZINAZOVUMA:

Trump kupanda kizimbani leo

Raisi wa zamani wa Marekani Donald Trump Leo atapandishwa kizimbani...

Share na:

Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump na washtakiwa wenzake 18 akiwemo wakili wake Rudy Giuliani na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi wa nchi hiyo, Mark Meadows wanatarajiwa kusomewa mashtaka yao leo Jumatatu Agosti 28, 2023 kwa mara ya kwanza.

Trump anakabiliwa na mashtaka ya tuhuma za kuingilia uchaguzi wa Georgia kwa madai ya kutafuta kura 11,000 za kumzidi aliyekuwa mpinzani wake katika uhaguzi wa mwaka 2021, Joe Biden.

Miongoni mwa mashahidi wanaosubiriwa kutoa ushahidi siku ya leo ni pamoja na Katibu wa Jimbo la Georgia Brad Raffensperger, ambaye anadaiwa kupokea simu Januari 2021 kutoka kwa Trump kwa ajili ya kuombwa amtafutie kura ili ashinde katika uchaguzi huo.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya