Baada ya kukamilisha usajili uongozi wa klabu ya soka ya Simba hii leo imeanza kutangaza wachezaji ambao wamewasajili kuelekea msimu mpya wa 2023/2024.
Mchezaji wa kwanza kutambulishwa ni kiungo mshambuliaji Willy Essomba Onana mwenye miaka 23 raia wa Cameron.
Onana amesajiliwa kutoka Rayon Sports ya Rwanda ambapo msimu uliopita aliibuka mchezaji bora wa ligi kuu nchini humo.
Onana amesaini ‘kandarasi’ ya miaka miwili kuwatumikia wababe hawa wa Tanzania.
Aidha wakati huo pia klabu ya soka ya Yanga Jana usiku imetangaza mchezaji wake wa kwanza ambae ni Mtanzania Nickson Kibabage akitokea klabu ya Singida Fountain Gate zamani ikifahimika kama Singida Big Stars.