ZINAZOVUMA:

Ruto ataka Afrika iungane

Raisi wa Kenya William Ruto amesikitishwa na Afrika ya Miongo...

Share na:

Rais William Ruto amesema inawezekana kujenga Afrika iliyounganishwa zaidi, yenye ustawi na utulivu huku akiongeza kuwa ilikufanikiwa ni lazima iendeshwe na Afrika na watu wake, viongozi na rasilimali zake.

Wito wa kuwepo kwa Muungano wa Afrika (AU) wenye nguvu umepigiwa debe katika mkutano wa tano wa uratibu wa nusu mwaka wa Umoja wa Afrika uliofanyika jijini Nairobi.

Mkutano huo uliongozwa na Rais wa Kenya. William Ruto ambaye alitoa wito wa mageuzi ya AU yanayozingatia uhuru wa kifedha kwa Muungano huo.

Rais William Ruto amesema inawezekana kujenga Afrika iliyounganishwa zaidi, yenye ustawi na utulivu huku akiongeza kuwa ilikufanikiwa ni lazima iendeshwe na Afrika na watu wake, viongozi na rasilimali zake.

Aidha Rais Ruto alisema kuwa hatua ya kuanzia inapaswa kuwa mageuzi ya Umoja wa Afrika. Alisikitika kwamba zaidi ya miongo mitano baada ya uhuru, bara bado linategemea ufadhili kutoka nje kuendesha ajenda zake.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya