ZINAZOVUMA:

Odinga kumshtaki Raisi Ruto

Raila Odinga amesema atakwenda mahakamani kumshtaki Raisi William Ruto kwa...

Share na:

Kongozi wa Umoja wa Azimio, Raila Odinga amesema anachukua uamuzi wa kumshtaki mahakamani Raisi wa Kenya, William Ruto ambaye ameunda Kamati ya kuchukunguza miili 110 iliyofukuliwa katika eneo la Shakahola lilipo katika Kanisa la “Good News International Church”, ambapo takribani Watu 320 wameripotiwa kupotea.

Uamuzi huo umekuja siku moja baada ya Polisi kumzuia Odinga na wasaidizi wake kuingia katika eneo la tukio.

Odinga amesema
“Rais hana uwezo ya kuunda jopo la uchunguzi, hiyo ni kazi ya Bunge na Bunge lenyewe limelala halijafanya hiyo kazi hivyo nitamshitaki Ruto kwa kukiuka Katiba”

Aidha Odinga amesema watuhumiwa walionekana wakisali pamoja na viongozi wa Taifa, hivyo Serikali haiwezi kujichunguza tukio ambalo nao wanahusika.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya