ZINAZOVUMA:

Ni ngumu kulikomboa Bara la Afrika kama yasipofanyika haya

Raisi Samia Suluhu Hassani amesema ni ngumu kulikomboa Bara la...

Share na:

Rais Samia Suluhu Hassan amesema ni muhimu kwa viongozi wa Afrika kuhakikisha wanaangalia, wanatathmini na kusimamia mageuzi yote muhimu ili kuliwezesha bara hilo kutumia uwezo na rasilimali zake kujikomboa kiuchumi.

Akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali Watu uliofanyika jijini Dar es Salaam, amesema bara la Afrika bado linahitaji mageuzi makubwa katika nyanja zote muhimu za uzalishaji na maendeleo, na kwamba idadi kubwa ya vijana iliyopo Afrika inaweza kutumika kama fursa ya kipekee kwa ajili ya mageuzi ya kiuchumi.

Aidha, Rais Samia amesema bara la Afrika halitajikomboa kiuchumi ikiwa nguvu kubwa haitaelekezwa kwenye maendeleo ya rasilimali watu kwa kutoa ujuzi na maarifa yanayohitajika.

“Hatuwezi kulikomboa bara letu kiuchumi kama hatutaelekeza nguvu zetu kwenye maendeleo ya rasilimali watu kwa kuwapa maarifa na ujuzi unaohitajika katika kuyatumia na kuyabadilisha mazingira yao kwa manufaa yao,” amesema Rais Samia Suluhu.

Endelea Kusoma

Mwanzilishi wa Telegram mwenye asili ya kirusi amekamatwa nchini Ufaransa siku ya

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya