ZINAZOVUMA:

Mwenge wazindua miradi Dar es salaam

Mwenge wazindua miradi mbalimbali yenye thamani zaidi ya bilioni 9...

Share na:

Jumla ya miradi sita yenye thamani ya Sh9 bilioni inatarajiwa kukaguliwa na kuzinduliwa kwenye mbio za Mwenge wa Uhuru utakaokimbizwa katika Wilaya ya Kigamboni.

Mwenge huo unakimbizwa leo Alhamisi Mei 25,2023 katika Wilaya hiyo ukitokea Temeke ambapo ulikagua na kuzindua miradi sita iliyogharimu Sh13 bilioni.

Jana Mwenge wa Uhuru uliwasili jijini Dar es Salaam ukitokea Mafia mkoani Pwani na kukabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila.

Hata hivyo akipokea Mwenge huo Chalamila alisema, utakimbizwa katika Wilaya zote za Dar es Salaam na kuzindua miradi 32 itakayogharimu Sh96 bilioni.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya