ZINAZOVUMA:

Msaidizi wa Xi Jinping azuiliwa kuingia kwenye mkutano wa BRICS

Msaidizi aliyeambatana na Rais wa China Xi Jinping alizuiliwa kuingia...
Chinese President Xi Jinping takes his oath after he is unanimously elected as President during a session of China's National People's Congress (NPC) at the Great Hall of the People in Beijing, Friday, March 10, 2023. Chinese leader Xi Jinping was awarded a third five-year term as president on Friday, putting him on track to stay in power for life. (AP Photo/Mark Schiefelbein)

Share na:

Wasaidizi wa Rais wa China, Xi Jinping jana Jumatano Agosti 23, 2023 wameripotiwa kuzuiwa kuingia katika ukumbi wa mkutano wa Brics unaofanyika jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Video fupi inayosambaa katika mitandao ya kijamii inaonyesha kuwa Xi Jinping alipokuwa akiingia ukumbini mtu anayedaiwa kuwa afisa wa usalama wa China alimfuata ili kuingia nae lakini alizuiwa mlangoni na maafisa wa usalama wa Afrika Kusini.

Ingawa kwa sasa haijulikani ni nini kilisababisha mkanganyiko huo, baadhi ya ripoti zimedokeza kwamba afisa huyo wa usalama alikuwa mtafsiri rasmi wa Rais Xi.

Mkutano wa Brics unahusisha Marais wa nchi wanachama ambazo ni Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini ambapo Rais wa Russia, Vladimir Putin kutokana na sababu za kiusalama amehudhuria mkutano huo kwa njia ya video.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya