ZINAZOVUMA:

Mechi Singida na Simba, mguu nje mguu ndani

TFF imesema kuwa klabu ya Simba na Singida Fountain Gate...

Share na:

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limesema klabu za Singida Big Stars na Simba SC mpaka sasa ndio Klabu pekee ambazo hazijawasilisha kibali cha mchezaji yoyote wa kigeni.

Aidha TFF iliweka wazi toka jana kuwa hakuna mchezaji atakayeruhusiwa kucheza mashindano ya Ngao ya Jamii kama hatakuwa amekamilisha taratibu za kisheria.

Pia TFF imezitaja klabu za Young Africans na Azam FC ndizo Klabu pekee zilizowasilisha vibali vya wachezaji wao wa kigeni.

Young Africans wamewasilisha vibali vya wachezaji 12 wakati Azam FC wamewasilisha vibali vya wachezaji 11.

Swali ni je leo mechi ipo au haipo?

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya