ZINAZOVUMA:

Malaria itibiwe bure nchi nzima

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amewataka wananchi wote kuhakikisha wanatibiwa...

Share na:

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amewataka wananchi kote nchini kuhakikisha wanatibiwa bure ugonjwa wa malaria na wasikubali kulipa fedha yoyote kupata vipimo, matibabu ikiwemo dawa au sindano.

Amesema kumekuwa na uhuni unaendelea katika vituo vya afya huku akisisitiza kuwa matibabu yote ya ugonjwa wa Malaria yanatolewa bure kwakuwa dawa zake zipo katika miradi misonge.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo Jumatano, Agosti 9, 2023 akiwa Temeke wakati akiendelea na ziara yake ya kutatua changamoto ya ufinyu wa maeneo unaozikabili hospitali na vituo vya afya mkoa wa Dar es Salaam.

“Wataalamu waache uhuni, dawa za Malaria zinapaswa kutolewa bure, bila malipo yoyote hii naisema wazi na wananchi wengi hawatambui hili, kuanzia kipimo cha haraka cha malaria, sindano ya Malaria kali na hata dawa ni za miradi misonge,” amesema Waziri Ummy.

Amesisitiza kuwa pia kuna dawa za watoto kuwakinga na kuharaka kundi lingine ni chanjo za watoto ambavyo hivyo vyote vinatolewa bure bila malipo yoyote.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya