ZINAZOVUMA:

Idadi yaongezeka wenye saratani chini ya miaka 50

Takwimu zinaonesha idadi ya wanaokumbwa na saratani kwa umri chini...

Share na:

Utafiti wa kimataifa uliochapishwa hivi karibuni kuhusu ugonjwa wa saratani unaonesha kuwa visa vya saratani vimeongezeka kwa watu wa chini ya miaka 50.

Kutoka idadi ya watu milioni 1.82 hadi watu milioni 3.26 katika kipindi cha miongo mitatu kwa wenye umri chini ya miaka 50 pekee.

Watafiti wametumia takwimu za tangu mwaka 2019 za uchunguzi uliofanywa na taasisi ya Global Burden of Disease iliyoainisha viwango vya aina 29 za saratani katika mataifa 204.

Watafiti hao wanasema, vichocheo vikubwa vya saratani kuwa ni ulaji mbaya na matumizi ya sigara na pombe kwa rika hilo, lakini wakikiri bado hakuna sababu ya wazi juu ya mwenendo wa ongezeko hilo ingawa ongezeko la idadi ya watu pia linachangia.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya