ZINAZOVUMA:

Bunge la Kenya lataka kusitisha mafao kwa Kenyatta

Bunge la Kenya linahitaji kura za kutosha ili kupitisha maamuzi...

Share na:

Bunge la Kitaifa la Kenya linahitaji kura za walio wengi kusitisha mafao ya kila mwezi na marupurupu mengine ya Rais wa zamani, Uhuru Kenyatta kwa kile kinachoelezwa anajihusisha na siasa baada ya kustaafu.

Mbunge wa Gatundu Kusini, Gabriel Kagombe aliwasilisha hoja katika Bunge la Kitaifa Jumanne iliyopita akitaka Kenyatta anyimwe marupurupu yake ya kustaafu.

Hoja hiyo pia inalenga kusitisha mafao na marupurupu mengine ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Odinga na aliyekuwa Makamu wa Rais, Kalonzo Musyoka.

Hoja hiyo inaungwa mkono kwa kiasi kikubwa na wabunge wanaounga mkono Muungano wa Kenya Kwanza wa Rais William Ruto.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya