ZINAZOVUMA:

Wachezaji wa kigeni Simba na Yanga kukosekana Tanga

Shirikisho la mpira Tanzania TFF limesema kuwa ni klabu ya...

Share na:

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limesema kuwa mpaka sasa Klabu ya Azam FC pekee ndio imewasilisha vibali vya wachezaji 10 wa kigeni ambao wanastahli kucheza kwenye michezo ya Ngao ya Jamii 2023, Tanga.

Wachezaji hao ni Ali Ahamada, Daniel Amoah, Kipre Junior, Prince Dube, Malickou Ndoye, Idrissu Abdulai, James Akamiko, Idiris Mbombo, Allasane Diao
Pamoja na Cheick Sidebe.

Klabu za Singida Fountain Gate, Simba SC na Young Africans bado hazijawasilisha vibali vya wachezaji wake wa kigeni.

Aidha TFF imesema hakuna mchezaji atakayeruhusiwa kucheza mashindano ya Ngao ya Jamii kama hatakuwa amekamilisha taratibu za kisheria.

Endelea Kusoma

Anguko la mfumo wa Crowdstrike umesababisha kapuni nyingi duniani kushindwa kutoa huduma

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya