ZINAZOVUMA:

Vicheko kwa watumiaji wa Petrol na dizeli

Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji EWURA...

Share na:

Furaha imetawala kwa watumiaji wa mafuta ya Petrol na dizeli kuanzia leo Julai 5 baada ya kushuka kwa bidhaa hizo katika mikoa inayochukua mafuta hayo bandari ya Dar es Salaam na Tanga ikilinganishwa na Juni.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) inaonyesha kuwa bei za mafuta kuanzia Julai 5, 2023 yale yanayochukuliwa bandari ya Dar es Salaam petroli imeshuka kwa Sh137 kwa lita na kuwa Sh2,736 huku dizeli ikishuka kwa Sh118 kwa lita na kuwa Sh2,544.

Kwa mikoa ya kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara) bei hiyo ya rejareja kwa mafuta ya petroli imeshuka kwa Sh188 kwa lita na kuwa Sh2,724 huku dizeli ikishuka kwa Sh58 kwa lita na kuwa Sh2,760.

Huku bei ikiendelea kusalia kwa mikoa ya kusini na ile inayochukua mafuta yake katika bandari ya Mtwara.

“Hakuna shehena ya bidhaa za mafuta iliyopokelewa kupitia Bandari ya Mtwara kwa Juni 2023. Hivyo basi, bei ya rejareja ya dizeli kwa mwezi Julai 2023 itaendelea kuwa ni ile iliyotangazwa katika toleo la tarehe 7 Juni 2023,”imesema taarifa hiyo.

Endelea Kusoma

Mwanzilishi wa Telegram mwenye asili ya kirusi amekamatwa nchini Ufaransa siku ya

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya