ZINAZOVUMA:

Raisi wa Kenya aondoa marufuku ya ukataji miti

Raisi wa Kenya William Ruto ameondoa marufuku ya ukataji miti...
This young man works for three years in the illegal lodging industry. Sleeping in a special camp in the forest to be able to cut as many trees as possible. They know the forest very well, at the same time their chainsaw is rapidly destroying the entire Ituri forest. Foto: Jan-Joseph Stok

Share na:

Rais wa Kenya, William Ruto ameondoa marufuku ya ukataji miti iliyokuwa imewekwa nchini humo kwa miaka sita iliyopita akisema marufuku hiyo iliathiri watu wengi waliokuwa wakitegemea mbao kama chanzo cha mapato.

Ruto ametoa kauli hiyo jana Jumapili Julai 2, 2023 mjini Molo ambapo amesema kuwa kuna haja ya kubuni nafasi za kazi na kufungua sekta za uchumi zinazotegemea mazao ya misitu.

Kuondolewa kwa marufuku hiyo kunakuja wakati Serikali ya Kenya ikiendelea na mpango wake wa kupanda miti bilioni 15 katika kipindi cha miaka 10 ili iweze kuongezeka nchini humo.

Mwaka 2018 Serikali ya Kenya ilipiga marufuku ukataji miti kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Endelea Kusoma

Mwanzilishi wa Telegram mwenye asili ya kirusi amekamatwa nchini Ufaransa siku ya

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya