ZINAZOVUMA:

Kenya: Mapya yaibuka mauaji ya Shakahola

Waziri wa Mambo ya ndani nchini Kenya amesema mchungaji Mackenzie...

Share na:

Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Kenya, Prof. Kithure Kindiki amesema mhubiri mwenye utata, Paul Mackenzie wa kanisa la Good News International Church aliajiri watu wenye silaha kuwachunga wafuasi wake kufunga mpaka pale watakapokufa kwa njaa.

Akizungumza mbele ya kamati ya Seneti inayochunguza tukio hilo siku ya Ijumaa, amesema Mackenzie alitumia genge lililomiliki silaha za jadi kuwaua baadhi ya waumini waliochukua muda mrefu kufa na wale waliobadilisha mawazo yao wakati wa kufunga.

“Mackenzie alikuwa ameajiri vijana wenye silaha ili kuzunguka wafuasi wake na kusimamia njaa yao hadi kufa. Wafuasi waliobadili mawazo yao kuhusu njaa waliuawa kwa kunyongwa au kupigwa na vitu butu,” amesema.

Hata hivyo amesema katika uchunguzi uliofanywa umebaini watu hao walilishwa vizuri, milo mitatu kwa siku, tofauti na ambavyo aliwaagiza waumini wa kanisa lake.

Endelea Kusoma

Mwanzilishi wa Telegram mwenye asili ya kirusi amekamatwa nchini Ufaransa siku ya

Chaguo la Mhariri

Habari Mpya